Psalms 131

Kumtegemea Mungu Kwa Unyenyekevu

(Wimbo Wa Kwenda Juu. Wa Daudi.)


1 aMoyo wangu hauna kiburi, Ee Bwana,
macho yangu hayajivuni;
sijishughulishi na mambo makuu kunizidi
wala mambo ya ajabu mno kwangu.

2 bLakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,
kama mtoto aliyeachishwa kunyonya
ndivyo ilivyo nafsi iliyoko ndani yangu.


3 cEe Israeli, mtumaini Bwana
tangu sasa na hata milele.
Copyright information for SwhKC